HABARI MOTO MOTO ...

Monday, November 12, 2012

Bomoabomoa Ubungo Kibangu kuanza leo

Nyumba zilizopo Ubungo Kibangu katika Kata ya Makubuli, jijini Dar es Salaam zitaanza kubomolewa kuanzia leo kwa lengo la kuendeleza mradi wa ujenzi wa barabara. Serikali kupitia Manispaa ya Kinondoni imeagiza kuwa wananchi na wafanya biashara walio katika eneo hilo waondoke kabla ya zoezi hilo kuanza. Kauli hiyo ilitolewa juzi jijini Dar es Salaam, na Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa, Desdery Ishengoma, wakati akizungumza na wakazi wa eneo hilo. Ishengoma alisema ujenzi huo unatarajia kuanza mara baada ya nyumba hizo kubomolewa. Alisema serikali ilishawalipa madai yao na ilitoa siku 60 kwa lengo la kuwataka waondokea katika eneo hilo na kutafuta maeneo mengine ya kuishi na kwamba baadhi ya watu walikwishaondoka kupisha mradi huo. “Kuanzia sasa hadi kufikia Jumatatu (leo) muda wowote tingatinga litapita kubomoa hizi nyumba zote zenye alama katika eneo hili kwa sababu muda uliotolewa umekwishamalizika na malipo walishalipwa na selikali,” alisema Ishengoma. Aliongeza kuwa barabara hiyo itawanufaisha wananchi wa eneo hilo kwa kupunguza msongamano pamoja na athari za mafuriko yanayotokea mara kwa mara kwa kujenga mifereji mirefu na mikubwa.

No comments:

Post a Comment