WILAYA ya Magu iliyopo jijini Mwanza, imetajwa kuwa ni moja kati
ya wilaya saba za jiji hilo zinazoongoza kwa mauaji ya watu wenye
ulemavu wa ngozi (Albino), wazee na vikongwe.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumapili, wilaya hiyo imekuwa ni moja ya wilaya zinazoongoza kwa matukio ya mauaji ya vikongwe na watu hao wenye ulemavu wa ngozi, jambo linalokiuka haki za binadamu na utawala bora.
Takwimu za kiuchunguzi zinaonesha kwamba, tangu mwaka 2005 hadi Septemba 2012, idadi ya vikongwe waliouawa walikuwa ni 267, wakati albino waliouawa walifikia 68.
Akithibitisha kuwepo kwa tatizo hilo la mauaji hayo, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jacqueline Liana, alisema licha ya kuwepo kwa mauaji hayo, lakini serikali imeweka mikakati ya kumaliza tatizo hilo huku watuhumiwa wa mauaji hayo wakikamatwa na kufikishwa mahakamani.
Mkuu huyo wa wilaya alisema mauaji hayo yanasababishwa na visa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na imani za kishirikina, ambapo hadi sasa watu 2,183 walishakamatwa na kuhojiwa kutokana na kudaiwa kuhusika katika mauaji hayo na 1,599 walifikishwa mahakamani.
Alisema kutokana na matukio hayo serikali imekuwa ikijitahidi kuchukua hatua za kuwakamata watuhumiwa wanaofanya vitendo hivyo, lakini jamii imekuwa kikwazo kwa kushindwa kutoa ushahidi pindi unapohitajika.
Liana alisema kuwa watu wengi wamekuwa waoga wa kutoa ushirikiano kwa viongozi na vyombo vya dola kwa kuwa wengi wana imani ya kwamba endapo watatoa ushahidi ndugu wa watuhumiwa wanaweza kuwaua, huku uelewa mdogo ukichangia kuwepo kwa tatizo hilo.
“Kwa huku kwetu Magu ipo hofu miongoni mwa jamii kuwa ukisimama mahakamani ukatoa ushahidi, kama kuna mianya ya rushwa kati ya hakimu na mtuhumiwa, basi shahidi anaweza kugeukwa na akatupwa jela kwa kusingiziwa kutoa ushahidi wa uongo,” alisema.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumapili, wilaya hiyo imekuwa ni moja ya wilaya zinazoongoza kwa matukio ya mauaji ya vikongwe na watu hao wenye ulemavu wa ngozi, jambo linalokiuka haki za binadamu na utawala bora.
Takwimu za kiuchunguzi zinaonesha kwamba, tangu mwaka 2005 hadi Septemba 2012, idadi ya vikongwe waliouawa walikuwa ni 267, wakati albino waliouawa walifikia 68.
Akithibitisha kuwepo kwa tatizo hilo la mauaji hayo, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jacqueline Liana, alisema licha ya kuwepo kwa mauaji hayo, lakini serikali imeweka mikakati ya kumaliza tatizo hilo huku watuhumiwa wa mauaji hayo wakikamatwa na kufikishwa mahakamani.
Mkuu huyo wa wilaya alisema mauaji hayo yanasababishwa na visa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na imani za kishirikina, ambapo hadi sasa watu 2,183 walishakamatwa na kuhojiwa kutokana na kudaiwa kuhusika katika mauaji hayo na 1,599 walifikishwa mahakamani.
Alisema kutokana na matukio hayo serikali imekuwa ikijitahidi kuchukua hatua za kuwakamata watuhumiwa wanaofanya vitendo hivyo, lakini jamii imekuwa kikwazo kwa kushindwa kutoa ushahidi pindi unapohitajika.
Liana alisema kuwa watu wengi wamekuwa waoga wa kutoa ushirikiano kwa viongozi na vyombo vya dola kwa kuwa wengi wana imani ya kwamba endapo watatoa ushahidi ndugu wa watuhumiwa wanaweza kuwaua, huku uelewa mdogo ukichangia kuwepo kwa tatizo hilo.
“Kwa huku kwetu Magu ipo hofu miongoni mwa jamii kuwa ukisimama mahakamani ukatoa ushahidi, kama kuna mianya ya rushwa kati ya hakimu na mtuhumiwa, basi shahidi anaweza kugeukwa na akatupwa jela kwa kusingiziwa kutoa ushahidi wa uongo,” alisema.
No comments:
Post a Comment