HABARI MOTO MOTO ...

Tuesday, November 27, 2012

Wanafunzi wamlipua Mkurugenzi Ustawi wa Jamii

Serikali imeombwa kumwondoa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Mbonimpaye Mpango kwa madai kwamba anawashawishi wanafunzi kumkataa Mkuu wa Chuo hicho, Abuu Mvungi.

Ombi hilo lilitangazwa na Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo hicho, Frank Nkinda, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam.

Alisema kumekuwa hakuna maelewano mazuri kati ya Mkurugezi na Mkuu wa chuo kitendo ambacho kinawaumiza wanafunzi.

“Sisi Wanafunzi tunatamka Mpango maarufu kama mama mpango kuondoka chuoni hapa kwa kuwa amekuwa mwiba na chanzo cha migogoro,” alisema Nkinda.

Alisema Mpango amekuwa akikwamisha shughuli za wanafunzi kwa kupandisha ada kiholela kwa lengo la kuifanya Taasisi ikose wanafunzi ili utendaji wa Mkuu wa taasisi uonekane mbovu.

Nkinda alisema kutokana na hila hizo Mkurugenzi huyo amekuwa akipeleka taarifa za uongo serikalini kuwa wanafunzi hawamtaki mkuu, kumbe yeye ndiye mwenye matatizo ya kutoelewana naye.

NIPASHE ilimtafuta Mkurugezi wa Chuo hicho kwa njia ya simu ili kujua juu ya tuhuma hizo, simu haikupokelewa wala ujumbe mfupi wa maandishi haukujibiwa.

NIPASHE ilipomtafuta Mkuu wa Chuo hicho simu zake zote za mkononi hazikupatikana.

No comments:

Post a Comment