Ajali mbaya imetokea eneo la bondeni, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam baada ya daladala ya Mwenge Kariakoo kukosa break na kugonga magari mawili na bajaji mbili. Katika ajali hiyo mama mmoja amegongwa vibaya na amekimbizwa hospitali ya Lugalo kwa matibabu.
Hali haikuwa nzuri maana kila mmoja alikuwa katika hali ya taharuki.
Bajaji zikiwa zimegongwa vibaya
Hapa
jijini Phoenix, mzazi mmoja (mama) na rafiki yake wa kiume
wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mtoto wa
miaka minne.
Msemaji wa Polisi bwana James Holmes amesema maofisa waliofika nyumbani kwa wawili hao juzi, siku ya Jumapili, punde baada ya mama huyo alipopiga simu ya dharura ya 911 kutoa taarifa ya kuomba msaada, walimkuta mtoto hapumui.
Mama huyo ambaye ni kijana wa miaka 19, Melissa Centeno alisema mwanaye alipigwa tumboni usiku wa Ijumaa na
Msemaji wa Polisi bwana James Holmes amesema maofisa waliofika nyumbani kwa wawili hao juzi, siku ya Jumapili, punde baada ya mama huyo alipopiga simu ya dharura ya 911 kutoa taarifa ya kuomba msaada, walimkuta mtoto hapumui.
Mama huyo ambaye ni kijana wa miaka 19, Melissa Centeno alisema mwanaye alipigwa tumboni usiku wa Ijumaa na
baada ya hapo akaanza kulalamika maumivu ya tumbo.
Rafiki wa Mellisa mwenye umri wa miaka 22, Sergio Ortiz amewambia maafisa kuwa alimchapa marehemu binti huyo mwishoni mwa juma hadi akaanguka kwenye karo la kuogea na kuchubuka usoni. Lakini, maofisa waliofanya uchunguzi wamesema kuwa sehemu na idadi ya michubuko katika mwili wa marehemu haiendani na maelezo ya watuhumiwa.
Sasa hivi wapo mikononi mwa polisi wakisubiri kusomewa mashitaka baada ya vipimo vya kitaalamu kufanyika.
Kisa hiki kinasikitisha mno kwani waliotenda kosa nao ni miaka michache tu walivuka umri wa utoto. Ikiwa Melissa ana umri wa miaka 19 kwa sasa, ina maana alimzaa mwanaye akiwa na umri wa miaka 15 hivi. Rafiki yake wa kiume (ambaye si baba mtoto) ana miaka 22. Nadhani huenda hawa hakuwa wamepevuka kiasi cha kutosha kubeba majukumu ya uzazi na malezi bora, ikizingatiwa kuwa wanaishi kaitka jamii ambayo mtoto akishavuka umri wa miaka 18, kisheria --ikiwa kila kitu kipo sawa-- anakuwa na haki ya kufanya maamuzi yake bila kuingiliwa na mzazi (ikiwa ni pamoja nahaki ya mwanaye, labda wazazi au au mzazi mwenza athibitishe kwa vielelezo kuhusu mapungufu ya mama huyo kumtunza mjukuu/mtoto) na kwenye mfumo wa maisha ambapo kila mtu anajijali kivyake (mind your own business, everybody for themselves and God for us all).
Jukumu la wazazi na walezi kuwa waangalizi au jamii kama kijiji kusaidiana kulea na kumkuza mtoto ni dhana iliyosahaulika kwa nyakati hizi ambazo mtoto ni mali ya Serikali na mwanangu ni wangu, ole wako umguse!
Hiki si kisa cha kwanza, na si kigeni lakini kutokana na visa hivi kujirudia, nimewaza na kutafakari nilivyolelewa na kujiuliza endapo si kwa jitihada na ushirikiano wa familia na wanakijiji, ningekuwa wapi? Wazazi wetu walikosea? Kama ndiyo, sisi tunarekebishaje? Kama siyo, kwa nini tumeupa kisogo utamaduni wa "It takes a village to raise a child"?
Rafiki wa Mellisa mwenye umri wa miaka 22, Sergio Ortiz amewambia maafisa kuwa alimchapa marehemu binti huyo mwishoni mwa juma hadi akaanguka kwenye karo la kuogea na kuchubuka usoni. Lakini, maofisa waliofanya uchunguzi wamesema kuwa sehemu na idadi ya michubuko katika mwili wa marehemu haiendani na maelezo ya watuhumiwa.
Sasa hivi wapo mikononi mwa polisi wakisubiri kusomewa mashitaka baada ya vipimo vya kitaalamu kufanyika.
Kisa hiki kinasikitisha mno kwani waliotenda kosa nao ni miaka michache tu walivuka umri wa utoto. Ikiwa Melissa ana umri wa miaka 19 kwa sasa, ina maana alimzaa mwanaye akiwa na umri wa miaka 15 hivi. Rafiki yake wa kiume (ambaye si baba mtoto) ana miaka 22. Nadhani huenda hawa hakuwa wamepevuka kiasi cha kutosha kubeba majukumu ya uzazi na malezi bora, ikizingatiwa kuwa wanaishi kaitka jamii ambayo mtoto akishavuka umri wa miaka 18, kisheria --ikiwa kila kitu kipo sawa-- anakuwa na haki ya kufanya maamuzi yake bila kuingiliwa na mzazi (ikiwa ni pamoja nahaki ya mwanaye, labda wazazi au au mzazi mwenza athibitishe kwa vielelezo kuhusu mapungufu ya mama huyo kumtunza mjukuu/mtoto) na kwenye mfumo wa maisha ambapo kila mtu anajijali kivyake (mind your own business, everybody for themselves and God for us all).
Jukumu la wazazi na walezi kuwa waangalizi au jamii kama kijiji kusaidiana kulea na kumkuza mtoto ni dhana iliyosahaulika kwa nyakati hizi ambazo mtoto ni mali ya Serikali na mwanangu ni wangu, ole wako umguse!
Hiki si kisa cha kwanza, na si kigeni lakini kutokana na visa hivi kujirudia, nimewaza na kutafakari nilivyolelewa na kujiuliza endapo si kwa jitihada na ushirikiano wa familia na wanakijiji, ningekuwa wapi? Wazazi wetu walikosea? Kama ndiyo, sisi tunarekebishaje? Kama siyo, kwa nini tumeupa kisogo utamaduni wa "It takes a village to raise a child"?































.jpg)












