HABARI MOTO MOTO ...

Tuesday, October 8, 2013

MGOMO WA MALORI NCHINI....MAFUTA YAANZA KUADIMIKA MBEYA


KUFUATIA mgogoro uliopo kati ya Serikali na wamiliki wa maroli nchini, mafuta ya Petrol na mafuta ya taa, yameanza kuadimika Jijini hapa. Imebainika.
Kikosi kazi cha mtandao wa www.geofreymtenzi.blogspot.com jana, lilitembelea baadhi ya vituo vya mafuta Jijini Mbeya na nje ya Jiji, na kuelezwa kuwa mgomo huo ukiendelea, huduma hiyo itasitishwa baada ya vituo hivyo kuishiwa mafuta kutokana na magari kutosafirisha bidhaa hiyo.
Baadhi ya wamiliki na wauzaji wa mafuta hayo, ambao waliomba hifadhi ya majina yao, walisema kuwa, madai yao ni ya msingi na kamati ya bunge ya miundombinu inayajua na ilikwisha yatolea maamuzi.
‘’Tunamshangaa Waziri Magufuli, tunajua anapata pasenti kupitia maamuzi yake kutoka kwa wakandarasi wa barabara na ndiyo maana anapuuza hata maagizo ya kamati ya Miundombinu iliyoketi Mjini Dodoma April 29, mwaka huu’’ walisema.
Moja ya barua ambayo aliandikiwa Mwenyekiti wa Tatoa May 16, mwaka huu, ambayo G MTENZI BLOG imeiona nakala yake, imesema kuwa, Tanroad wanafanya kazi kwa mazoea na uzembe .
‘’Jambo ambalo linaleta usumbufu na ucheleweshaji kwenye kusafirisha mizigo ya wateja na hivyo kuwa sababu ya wateja kukimbia kupitisha bidhaa bandari ya Dar es Salaam’’ imesema barua hiyo.
Sanjari na hayo, barua hiyo ambayo nakala yake ilipelekwa kwa Waziri wa Ujenzi na kupokelewa May 17, mwaka huu, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Tanroad Makao makuu na Tanroad Mkoa wa Dar es Salaam ikilalamikia suala la mizani.
Imeelezwa kuwa, mizani zinazotumika kupima magari yanayobeba mizigo mizito na abiria nchi Tanzania, zina mapungufu makubwa ambayo yanadhaniwa kuwa ni makusudi ya watendaji wa mizani hizo ili kujipatia fedha.
Mfano katika Mizani ya Kibaha May 11,05,2013, Mzigo uliopimwa na kupatikana na uzito wa Kgs 44.850, mizani ya Mikese ulipatikana na Kgs 39.900 na Kihonda Kgs 35.250 na hiyo ni gari hiyo hiyo moja.
Katika gari hiyo hiyo, siku iliyofuata katika Mizani ya Dodoma zilipatikana Kgs 46.759, mizani ya Singida ilikuta gari hiyo ikiwa na Kgs 38.600, Tinde Kgs 44.700 na Usagara Kgs 45.320.
Sanjari na hayo, taarifa iliyonukuliwa kutoka kwenye hotuba ya kambi ya upinzani. Sehemu hii inaonyesha ubadhirifu wa fedha kwenye wizara iliyoko chini ya Dr John Pombe Magufuli.
Mheshimiwa Spika,baada ya fedha hizi kupunguzwa kiasi cha shilingi bilioni 95 na kupelekwa wizara ya uchukuzi zilibakia kiasi cha shilingi bilioni 252.975.
Katika kifungu hiki, leo tumelazimika kulikumbusha Bunge kuhusiana na suala hili kwani kwa mujibu wa ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ya mwaka husika wa fedha kuhusiana na kifungu hiki alisema, naomba kunukuu
“malipo ya madeni ya mwaka wa nyuma yaliyolipwa kwa fedha za 2011/2012 kwa kutumia jina la mradi usiohalisi Tshs.252,975,000,000.
Miradi katika wizara ilipewa namba 4168 kwa ajili ya kupitisha malipo ya madeni ya miaka ya nyuma kwa miradi inayotekelezwa na TANROADS. Namba hii sio halisi''

No comments:

Post a Comment