Watu 70 wauawa.
Iraq. Jumla ya watu 73 wameuawa na wengine 100 wamejeruhiwa
katika shambulizi lililofanywa kwa mahujaji wa kishia katika mji mkuu wa
Irak, Baghdad.
Kwa mujibu wa maofisa wa Wizara ya Ndani,
mashambulizi hayo yalitokea katika Wilaya ya Adhamiyah wakati mahujaji
walipokuwa wanaelekea katika misikiti ya kishia.
Hata hivyo, hakuna kundi lolote ama mtu yeyote
aliyekiri kuhusika na mashambulizi hayo ya juzi . Umoja wa Mataifa
ulisema takriban watu 1000 waliuawa nchini Iraq katika mashambulizi
mwezi uliopita.
No comments:
Post a Comment