LONDON, England
KAULI ya Kocha Rafa Benitez kwamba kama angependekezwa kufundisha Chelsea, kwenye orodha ya makocha angesimama mwisho, leo inaweza kuzua jambo mbele ya mashabiki wa timu ya Chelsea aliyopewa jukumu la kuifundisha atakapowavaa mabingwa watetezi England, Manchester City.
KAULI ya Kocha Rafa Benitez kwamba kama angependekezwa kufundisha Chelsea, kwenye orodha ya makocha angesimama mwisho, leo inaweza kuzua jambo mbele ya mashabiki wa timu ya Chelsea aliyopewa jukumu la kuifundisha atakapowavaa mabingwa watetezi England, Manchester City.
Ni mtihani wa kwanza kwa Benitez tangu atwae mikoba ya kufundisha Chelsea, mabingwa hao wa Ulaya Jumatano iliyopita akichukua nafasi ya Kocha Roberto Di Matteo.
Benitez ana historia na mashabiki wa Chelsea, siyo kwa sababu yeye ni mtu anayeonekana anaweza kumfunika rekodi ya Kocha Jose Mourinho, bali namna alivyowahi kuwazungumzia.
Aliiongoza kwa mafanikio Liverpool na sasa ana Chelsea mpya yenye wachezaji kama Juan Mata, Oscar na Eden Hazard, ambao hawana mbinu za kuzuia na kuharibu.
Ni wazi kabisa, mashabiki wa Chelsea siyo rahisi kuvutiwa sana na Rafa, lakini wana mtu mwingine wa kuvutiwa naye. Huyu ni Brendan Rodgers.Kocha wa City, Roberto Mancini anaamini Chelsea itakuwa hatari zaidi baada ya kumwondoa Kocha Roberto Di Matteo.
Mabingwa hao watetezi wanakwenda Darajani leo kuikabili Chelsea itakayokuwa na kocha wa muda akiiongoza The Blues mara ya kwanza ndani ya siku tano tangu kupewa jukumu hilo.
Mancini, anayeamini kuwa Di Matteo hakuwa na bahati kwenye kazi yake, anasema Chelsea inaweza kufaidika kimchezo kutokana na mazingira ya kocha mpya.
"Kwa kawaida, timu inapobadilisha kocha, upande wa upinzani wanaocheza nao huwa mgumu," alisema Mancini. "Kwetu nadhani ni ngumu sana."
Mancini amesikitishwa kwa kocha mwenzake raia wa Italia kutimuliwa kazi, ambaye alikutwa na panga hilo baada ya The Blues kunyukwa mabao 3-0 na Juventus kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa.
"Nimesikitika kuondoka Di Matteo, yeye alishinda taji la Mabingwa wa Soka Ulaya miezi sita iliyopita. Siku zote maisha huwa hivyo" aliongeza.
"Tunapokuwa na chaguo la kazi hii, pia tunafahamu kwamba kwenye maisha lolote linaweza kutokea."
City wameipindua Chelsea kileleni mwezi huu na sasa wanaongoza msimamo, lakini bado anaamini kuwa wapinzani wao walikuwa wazuri chini ya Di Matteo.
"Kabla ya mechi tatu za mwisho, walionyesha mchezo mzuri na walikuwa kileleni mwa msimamo," alisema.
"Bado naamini Chelsea walikuwa wazuri chini ya Di Matteo na itakuwa timu nzuri zaidi ikiwa na Benitez. Wana wachezaji wazuri zaidi."
Benitez anaungana na mshambuliaji wake aliyemsajili na kumwacha Liverpool kabla ya kujiunga na Chelsea, Fernando Torres, ambaye Di Matteo alimweka benchi kwenye mechi ya Turin dhidi ya Juventus Jumanne iliyopita.
Torres amefunga mara moja tu katika mechi tatu za mwisho na Mancini anaongeza: "Nadhani Fernando ni mshambuliaji mzuri. Wakati mwingine ni vigumu kwa mshambuliaji kama hafungi mabao kama alivyo yeye."
No comments:
Post a Comment